Msola akikabidhi zawadi kwa wachezaji wa Neteboli
ripotiZAmitaa!!!!
Sunday, May 25, 2014
Saturday, May 24, 2014
JAMAA PANDE ZA IPOGOLO -IRINGA,KAPOTEZA UHAI BAADA YA KUZIDISHA POMBE,
MBALI ya jitihada mbalimbali
zinazofanywa na makampuni ya kutengeneza pombe kutoa tahadhari kuwa unywaji wa
pombe kupita kiasi ni hatari kwa afya, ‘janki’ Geoffrey Mlelwa (26), mkazi wa
Ipogolo mjini hapa, amejikuta akiyakatisha maisha yake kwa kudaiwa kugida pombe
kupindukia.Tukio hilo la kusikitisha lilijiri juzikati ambapo kijana huyo
alikuwa katika Soko Kuu la Manispaa ya Iringa akiwa na wenzake wakipiga ulabu
kwa staili ya kuchanganya (kuchoma sindano) ndipo Geoffrey alipopitiliza na
kusababisha apoteze uhai.
NI INDIRECT FIGHT KATI YA CCM NA CHADEMA IRINGA LEO.
MAWAZIRI watatu wako
mkoani Iringa na leo Mei 24 wanatarajia kushiriki kikao nyeti kinachohusu
mustakabali wa ujenzi wa stendi mpya ya mabasi yaendayo mikoani katika eneo la
Igumbilo.
Mawaziri hao ni
pamoja na Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe, Waziri wa Mazingira Dk
Benelith Mahenge na Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),
Hawa Ghasia.
Maamuzi
yatakayotolewa katika kikao hicho kitakachofanyika katika ukumbi wa manispaa ya
Iringa yatatoa majibu ambayo kwa namna moja au nyingine yataupa ushindi upande
fulani wa siasa.
Thursday, May 22, 2014
MSOLA ACHANGIA UJENZI WA KANISA LA KKKT NDENGISIVILI
MBUNGE jimbo la Kilolo, Profesa Peter
Msolla ametoa Sh 150,000 kama mchango wake kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa la
Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), usharika wa Ndengisivili, wilayani
Kilolo.
Wakati wakisubiri kukamilika kwa ujenzi
wa kanisa hilo, waumini zaidi ya 120 wa usharika huo wanaabudu katika jengo la
muda lililojengwa kwa tope huku likiwa limeezekwa kwa nyasi.
Saturday, May 10, 2014
MASANJA AWACHEFUA WAUMINI,,NI BAADA YA KUONEKANA AKICHATI WAKATI WA IBADA.
MSANII mahiri wa komedi ambaye pia ni Mwimbaji wa Injili,
Emmanuel Mgaya ‘Masanja’ amenaswa akichati kwenye simu wakati viongozi wa dini
wakishusha maombi mazito.
Tukio hilo lililowachefua baadhi ya waumini lilitokea hivi
karibuni katika Uwanja wa Shule ya Msingi Saba Saba, mjini Moro ambapo Masanja
aliyekuwa meza kuu, wakati wenzake wakiongoza sala ya kufungua kongamano hilo,
yeye alikuwa bize na simu.
Kitendo hicho kilidumu kwa dakika kadhaa kisha staa huyo ambaye
pia ana ndoto ya kuwa mchungaji mkubwa nchini, akajiunga na wachungaji wengine
waliokuwa meza kuu kuendelea na sala.
Subscribe to:
Posts (Atom)