Kuna taarifa zimeenea kwenye mitandao kuwa Naibu Katibu Mkuu Bara CHADEMA, Zitto ataanza safari ya kuimarisha chama katika mikoa 5 hapa nchini na kwamba inatokana na yeye 'kujitenga' na ziara inayoendelea hivi sasa ya Mabaraza Huru ya Katiba Mpya, kukiwa na timu mbili, chini ya viongozi wakuu wa kitaifa, Mwenyekiti Freeman Mbowe na Katibu Mkuu, Dkt. Willibrod Slaa, ambapo kila timu inatumia usafiri wa chopper!
Wana CHADEMA wawe makini na upotoshaji au hila za kuwaondoa kwenye focus ya suala la Katiba Mpya, hasa ambapo kwa sasa chama kinakusanya maoni ya wanachama na wapenzi wake juu ya Rasimu ya Katiba Mpya, kwenye mikutano ya hadhara inayoendelea nchi nzima.