Showing posts with label ZITTO KABWE. Show all posts
Showing posts with label ZITTO KABWE. Show all posts

Tuesday, August 27, 2013

ZITTO KUTOGOMBEA URAIS 2015

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Bw. Zitto Kabwe (CHADEMA), amesema hafikirii kugombea urais kwa tiketi ya chama hicho wala ubunge katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2015.

Alisema mwaka 2015, ndio mwaka wa mwisho kujihusisha na siasa ambapo dhamira yake ni kutafuta chuo ambacho ataweza kufundisha masomo ya uchumi na maliasili.

Monday, August 19, 2013

ZITOO KABWE AKANUSHA UVUMI ULIOENEA JUU YA KUJITENGA KWAKE NA HARAKATI ZA CHADEMA.


Kuna taarifa zimeenea kwenye mitandao  kuwa Naibu Katibu Mkuu Bara CHADEMA, Zitto ataanza safari ya kuimarisha chama katika mikoa 5 hapa nchini na kwamba inatokana na yeye 'kujitenga' na ziara inayoendelea hivi sasa ya Mabaraza Huru ya Katiba Mpya, kukiwa na timu mbili, chini ya viongozi wakuu wa kitaifa, Mwenyekiti Freeman Mbowe na Katibu Mkuu, Dkt. Willibrod Slaa, ambapo kila timu inatumia usafiri wa chopper!

Wana CHADEMA wawe makini na upotoshaji au hila za kuwaondoa kwenye focus ya suala la Katiba Mpya, hasa ambapo kwa sasa chama kinakusanya maoni ya wanachama na wapenzi wake juu ya Rasimu ya Katiba Mpya, kwenye mikutano ya hadhara inayoendelea nchi nzima.

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...