Kiongozi wa Jumuiya na Taasisi za
Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda leo amepandishwa kizimbani katika Mahakama
ya Hakimu Mkazi Mfawidhi mkoa wa Morogoro kujibu mashitaka matatu yanayomkabili
ambayo ni kutotii amri halali, kutoa maneno yenye nia ya kuharibu imani za dini
na kushawishi kutenda kosa.
Sheikh Ponda amefikishwa mjini
Morogoro na helkopta ya jeshi la polisi majira ya saa tano asubuhi chini
ya ulinzi mkali ambapo askari waliimarisha ulinzi kwa muda wote huku kikosi cha
kutuliza ghasia FFU wakiwa na silaha mabomu na mbwa ambapo hali hiyo imesababisha
kusimama kwa baadhi ya shughuli zingine za kiofisi katika ofisi zilizopo jirani
na mahakama ya hakimu mkazi wakati kesi hiyo ikiendelea ...



