KATIBU Mkuu wa Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Wilbroad Slaa leo Jumamosi atazindua
kampeni za uchaguzi mdogo jimbo la Kalenga, wilayani Iringa katika kijiji cha
Kalenga.
Kwa upande wao Chama
cha Mapinduzi (CCM) kitanzaa kampeni zake keshokutwa Jumapili katika kijiji cha
Mseke wakati kikiendelea na maandalizi ya uzinduzi rasmi wa kampeni hizo.



