HAYA ninayoyaandika leo katika safu hii
yanaweza kuwa si mageni. Inawezekana kabisa ni marudio ya
kilichokwishakuandikwa.
Huenda pia ni mambo yanayoudhi baadhi ya watu
ama kwa maudhui yake au kwa kurudiwarudiwa kwake. Mara nyingi kuhoji mazoea si
jambo linalopokewa vyema hasa na wale wasioona tatizo katika hali ilivyo
(status quo).
Leo ninapenda kudadisi kwa ukaribu zaidi hicho
ninachokiona huko tunakoelekea kama jamii ambako huenda si wengi wetu wanaoona
umuhimu wa kufanya hivyo. Kabla sijaingia katika udadisi huo nirejee kwa kifupi
utangulizi wangu ambao utaweka mawazo yangu ya leo katika muktadha wake kamili.
