MAWAZIRI watatu wako
mkoani Iringa na leo Mei 24 wanatarajia kushiriki kikao nyeti kinachohusu
mustakabali wa ujenzi wa stendi mpya ya mabasi yaendayo mikoani katika eneo la
Igumbilo.
Mawaziri hao ni
pamoja na Waziri wa Maji Profesa Jumanne Maghembe, Waziri wa Mazingira Dk
Benelith Mahenge na Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),
Hawa Ghasia.
Maamuzi
yatakayotolewa katika kikao hicho kitakachofanyika katika ukumbi wa manispaa ya
Iringa yatatoa majibu ambayo kwa namna moja au nyingine yataupa ushindi upande
fulani wa siasa.

