Kiongozi wa Jumuiya na Taasisi za
Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda leo amepandishwa kizimbani katika Mahakama
ya Hakimu Mkazi Mfawidhi mkoa wa Morogoro kujibu mashitaka matatu yanayomkabili
ambayo ni kutotii amri halali, kutoa maneno yenye nia ya kuharibu imani za dini
na kushawishi kutenda kosa.
Sheikh Ponda amefikishwa mjini
Morogoro na helkopta ya jeshi la polisi majira ya saa tano asubuhi chini
ya ulinzi mkali ambapo askari waliimarisha ulinzi kwa muda wote huku kikosi cha
kutuliza ghasia FFU wakiwa na silaha mabomu na mbwa ambapo hali hiyo imesababisha
kusimama kwa baadhi ya shughuli zingine za kiofisi katika ofisi zilizopo jirani
na mahakama ya hakimu mkazi wakati kesi hiyo ikiendelea ...
Akisoma shataka mbele ya hakimu
mkazi Richard Kabate , wakili mkuu wa serikali kanda ya Morogoro Benard
Kongola amedai kuwa shekh Ponda anadaiwa kutenda makosa hayo matatu Agosti 10
mwaka huu majira ya jioni katika viwanja vya shule ya msingi kiwanja cha ndege
manispaa ya Morogoro.
Katika shitaka la kwanza la
shekhe Ponda anadaiwa kutotii amri halali ambapo shitaka la pili anadaiwa
kutoa maneno yenye nia ya kuharibu imani za dini kwa kutoa maneno kuwa serikali
iliamua kupeleka jeshi Mtwara kushughulikia suala la vurugu iliyotokana
na gesi kwa kuwaua na kuwatesa wananchi kwa sababu asilimia 90 ya wakazi wa
Mtwara ni Waislamu.
No comments:
Post a Comment