KATIBU Mkuu wa Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Wilbroad Slaa leo Jumamosi atazindua
kampeni za uchaguzi mdogo jimbo la Kalenga, wilayani Iringa katika kijiji cha
Kalenga.
Kwa upande wao Chama
cha Mapinduzi (CCM) kitanzaa kampeni zake keshokutwa Jumapili katika kijiji cha
Mseke wakati kikiendelea na maandalizi ya uzinduzi rasmi wa kampeni hizo.
Uchaguzi huo
unakishirikisha chama kingine cha Chausta kilichomsimamisha Richard Minja
kupeperusa bendera yake.
CCM kwa upande wao
imemsimamisha, Godfrey Mgimwa, huku Chadema ikiwa imemsimamisha Grace Tendega.
Kwa mujibu wa
taarifa iliyotolewa na Msimamizi wa Uchaguzi wa Wilaya ya Iringa, Pudenciana
Kisaka, jimbo la Kalenga lina jumla wapiga kura 85,051.
Akizungumza na www.frankleonard.blogspot.com Katibu
wa Chadema Iringa Vijijini, Felix Nyondo alisema Dk Slaa atawasilia mjini
Iringa kwa gari mapema kesho katika mapokezi yatakayohusisha msafara mkubwa wa
magari na pikipiki katika eneo la Ndiuka mjini hapa.
Mbali na Dk Slaa,
Nyondo alisema wengine watakaokuwepo kwenye uzinduzi wa kampeni hizo ni Mbunge
wa Arusha Mjini, Godbless Leman na viongozi mbalimbali wa chama hicho.
Alisema baada ya
uzinduzi huo, Chadema itaendelea na kampeni za kila siku na kwa mujibu wa
ratiba yao, kila siku watakuwa wakifanya mikutano 39.
Nyondo alisema
katika kampeni hizo Chadema itatumia helkopta (chopa) tatu, magari 56 na
pikipiki 80.
Alisema vyombo hivyo
vya usafiri vitagawanywa katika kata zote 13 za jimbo hilo ili kufanikisha
shughuli nzima ya kampeni zao.
Kaimu Katibu Mkuu wa
CCM Mkoa wa Iringa, Hassana Mtenga alisema CCM kwa upande wake inaendelea na
maandalizi ya uzinduzi rasmi wa kampeni zake.
Katika uzinduzi huo
ambao hata hivyo hakutaja tarehe yake, alisema viongozi mbalimbali wa CCM ngazi
ya Taifa, Mkoa na wilaya watashiriki.
“Kabla ya uzinduzi
huo tutakuwa mikutano kadhaa, mikutano hiyo tunaiita ya rasharasha kabla
shughuli nzito haijaanza; kwa kuanzia tutafanya mkutano wetu wa kwanza katika
kijiji cha Mseke, Jumapili keshokutwa,” alisema.
No comments:
Post a Comment