Monday, August 26, 2013

NIKK MBISHI NI MUATHIRIKA WA UKIMWI!!!!??


Tumekuwa  tukishuhudiwa  vituko  mbalimbali  vya  wasanii wetu  ambao  wamekuwa  wakihangaika  usiku  na  mchana  kuusaka  umaarufu....

Wapo  ambao  wamekuwa  wakivua  nguo  zao  jukwaani, wapo  ambao  wamekuwa  wakipiga  picha  za  uchi  na  kuzitupia  mitandaoni.Yote  hiyo  ni  kutafuta  Jina  au  umaarufu ambao  mimi  binafsi  nauita  ni  umaarufu  wa  kishamba.....


Leo  Nick  Mbishi  ametoa  kituko  ambacho  kimenifanya  niamini  kuwa  wasanii  wetu  wana njia  mpya  kwa  sasa  za  kutaka kujulikana ( kuwa  maarufu).

Katika  account  yake  ya  Twitter, 
Nick  Mbishi  alitoa  post  moja  ikielezea  kuwa  yeye  ni  muathirika  wa  ukimwi.

Post  hiyo  ilikuwa  na  taswira  mbili  za mafumbo . Fumbo  la  kwanza  linamaanisha  kuwa  Yeye  NI  mwathirika  wa  UKIMWI  huku  fumbo  la  pili  likimaanisha  kinyume  chacke.

Baada  ya  post  hiyo, mijadala  kadhaa  ya  watu iliibuka  kwenye  mitanado  ya  jamii.Wapo waliompa  pole  na  wapo  waliompongeza  kwa  ujasiri  wake...

Cha  kushangaza  ni  kwamba, baada  ya  Nick  kuona kuwa issue  imekuwa  serious  kuhusu  madai  ya  yeye  kuwa  na  UKIMWI, alirudi  tena  Twitter  na  kuanza  kuilaumu  mitandao  ya  kijamii....

Kinachonishangaza  ni  kwamba, Nick  anakaumu  nini  wakati  alitamka  mwenyewe??.Hizo  ni  sifa  za  kishamba  za  kutaka  jamii  ikuongelee  na  kukujadili...

Kama  umeamua  kujitangaza, basi  kuwa  serious  ili  watu  wajue  moja.




No comments:

Post a Comment

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...